MAHUBIRI JUMAPILI, 02-10-2016, MCHG G . NKYA

Posted in Habari on Oct 05, 2016


Bwana wetu Yesu Kristo apewe sifa

Tunaendelea kuwakaribisha watu wote wa mataifa yote,Dini zote na kabila zote katika ibada za kila jumapili hapa Kanisani Usharikani KKKT Ubungo

Pia endelea kubalikiwa na mahubili ya kila jumapili kupitia website hii,Hapa chini ni summary ya mahubili ya jumapili ya tarehe 02.10.2016

NENO:Jina la Bwana ni Ngome Imara

Yoh 1:1-5

-Vitu vyote vimekuwepo hapa duniani ,vimekuwepo kwa sababu ya uwezo wa Yesu ,pasipo yeye hapakuwepo na kitu chochote

Mathayo 16:18-19

-Mistali hii inatuonyesha nia ya Yesu ya kujenga kanisa lenye nguvu na ambalo shetani hatoliweza

Waefeso 1:22-23

-Wakristo wengi hatujafahamu nguvu iliyopa katika jina la Yesu

Marko 16

-Kwa jina langu mtatoa pepo na hata mtakapokanyaga nge na nyoka hawatawadhulu

-Ukiwa na Jina la Yesu mwanadamu ni nani ata akutishe?

TUNACHOJIFUNZA:

Tusiende ibadani kwa ajili ya kufuata utaratibu tu, bali twende ibadani kwa vile yesu yupo hapo na atatuhudumia kwa mambo yote .

Kupitia jina la Yesu tutapata muafaka wa kila jambo kwenye maisha Yetu

Tunatakiwa kujua na kukumbuka kuwa jina la Yesu ni jina lipitalo majina yote